Header Ads

Raisi Vladmir Putin aingilia kati maandalizi ya kombe la dunia


Fainali za kombe la dunia mwakani zinapigwa nchini Urusi, mataifa mbali mbali hata wale ambao timu zao hazitashiriki kombe hilo watakuwepo nchinj Urusi kutazama michuano hiyo mikubwa zaidi duniani.
Kwa sasa imebaki miezi kadhaa tu twende Urusi lakini unaambiwa nchini humo bado sana yani ndio kwanzaaa wako nyuma sana katika maandalizi utafikiri mashindano hayo ni 2020.
Hali hii ya kusua sua kwa maandalizi imemkera raisi wa Urusi Vladmir Putin na kusema kwamba hawezi kukubali taifa lake kuonekana nyuma kutokana na uzembe wa watu wachache wa soka.
Putin amesema anaingiwa na hofu kwamba fainali hizo zitafika huku maandalizi yakiwa hayajakamilika jambo ambalo linaweza kuichafua nchi ya Urusi na kutoa sifa mbaya kwake.
Pamoja na kuandaa kombe la Shirikisho Fifa mwezi June lakini Urusi inaonekana bado viwanja vingi havijakamilika na bado sana hawajaweka mikakati kuhusu kukabiliana na wimbi la wageni watakaokwenda Urusi.
Michuano ya kombe la dunia inataraji kupigwa kuanzia June mwakani hadi July mwakani na tayari Urusi wameandaa kadi maalum kwa ajili ya usalama wa mashabiki watakaokuwa hapo.

No comments