Matokeo ya michezo yote ya EPL wikiendi hii
Hapo jana siku ya Jumapili michezo kadhaa imepigwa katika ligi kuu nchini Uingereza ambapo klabu ya Arsenal imechomoza na ushindi wa mabao 5-2 dhidi Everton ikiwa ugenini katika dimba la Goodison Park huku wenyeji wakiongozwa na Wayne Rooney wakishindwa kuokoa jahazi la timu hiyo lililokuwa likizama EPL.
Everton dhidi ya Arsenal 5-2
Katika matokeo ya michezo mingine Tottenham imechomoza na ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Liverpool katika dimba la Wembley.
Tottenham dhidi ya Liverpool 4-1
Michezo iliyopigwa siku ya Jumamosi ni
Na huko Stamford Bridge mabingwa watetezi wa ligi kuu ya nchini Uingereza klabu ya Chelsea imechomoza na ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Watford.
Chelsea dhidi ya Watford 4-2
Wakati kikosi cha mreno, Jose Mourinho klabu ya Manchester United hapo juzi siku ya Jumamosi imewashangaza wengi baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Huddersfield wakiwa ugenini na kuwa ndiyo mchezo wake wa kwanza kupoteza katika ligi ya Uingereza msimu huu.
Manchester United ikifungwa 2-1 dhidi ya Huddersfield
Klabu ya Manchester City imechomoza na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Burnley.
Manchester City ikiifunga Burnley mabao 3-0
Huko Newcastle klabu hiyo imeifunga timu ya Crystal Palace bao 1-0 lilifungwa na mchezaji, Mikel Merino.Stoke ikiwa nyumba imekubali kipigo cha mabao 2-1 dhidi ya Bournemouth magoli ya kifungwa na Andrew Surman na Junior Stanislas.
Newcastle imechomoza na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Crystal Palace
Wakati katika dimba la Liberty kikosi cha Leicester kimeifunga timu ya Swansea kwa jumla ya mabao 2-1 huku meneja wa timu hiyo, Michael Appleton akichomoza na ushindi wake wa kwanza toka aanze kukiongoza kikosi hicho.
Timu ya Southampton ikiwa nyumbani imechomoza na ushindi wa bao 1- 0 dhidi ya West Brom bao la dakika za mwisho la Sofiane Boufal likaipa ushindi.
Southampton ikiwa nyumbani imechomoza na ushindi wa bao 1- 0 dhidi ya West Brom
Post a Comment