Header Ads

Baraka The Prince Afunguka Kuhusu Kuondoka Rockstar4000 Amekiri Kumempa Changamoto Kubwa

Baraka The Prince Afunguka Kuhusu Kuondoka Rockstar4000 Amekiri Kumempa Changamoto Kubwa


Baraka The Prince ambaye sasa anajisimamia kupitia 'label' yake BANA MUSIC amekiri alipoachana na kampuni iliyokuwa inasimamia kazi zake ya Rockstar4000 kumempa changamoto kubwa kwani saizi kila kitu yeye ndiyo inabidi apambane tofauti na mwanzo.

Baraka The Prince amesema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha Friday Night Live (FNL) na kusema hata ukimya wake katika muziki kwa kipindi fulani ni kutokana na ukweli kwamba alikuwa anakutana na changamoto pamoja na kujipanga ili kuweza kurudi vizuri. 

No comments