Juventus moto mwingine
Juventus wameibuka katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na kuichapa Sporting Lisbon kwa mabao 2-1,Mabao ya Juventus yamefungwa na Maralem Pijanic na Mario Mandzukic huku lile la Sporting likifungwa na Alex Sandro aliyejifunga.
Matokeo hayo yameifanya klabu hiyo kuibuka katika mlolongo wa matokeo mabaya baada ya wikiendi iliyopita kupoteza katika uwanja wa nyumbani dhidi ya Lazio kwa mabao 2-1 huku Paul Dybala akikosa penati katika dakika za mwisho.
Post a Comment