Header Ads

Nandy amtaja anayemvutia ndani ya WCB


Msanii wa Bongo Flava na hitmaker wa wimbo ‘One Day’, Nandy amemtaja mshindi wa tuzo ya BET kutoka label ya WCB, Rayvanny kama msanii anayetamani kufanya nae kazi kutoka ndani ya label hiyo.
Muimbaji huyo ameeleza kuwa kwa namna anavyotazama aina ya muziki anaofanya Rayvanny na wake anaona unaendana, huku akiongeza kuwa Saida Karoli ni miongoni mwa wasanii wa kike ambao pia anatamani kurudia nyimbo zao.
“Nawaelewa wote lakini kwa haraka haraka nikipewa chance kwa mtu wa WCB kufanya nae ngoma nitafanya na Rayvanny. Nahisi kama tuna chemistry ile ambayo tunaweza tukaendana, yaani ukiwasikiliza mashairi yao wewe ndio unajua unafiti wapi, kwa hiyo mimi naona kwa Rayvanny nafiti,” ameiambia Clouds FM Top 20.
Kuhusu kufanya kazi na Saida Karoli, Nandy amesema, “natamani sana hata anipe ngoma yake ya zamani niifanyie remix na sijui ni ipi kwa sababu kafumua!, sijui nitaimbaje. Natamani anipe nifanye verse na kama alifanya chorus ibaki pale pale, halafu mimi nirudie zile verse, I hope atakubali,” amesisitiza.
Nandy ambaye kwa sasa anafanya vizuri na wimbo wake mpya ‘Wasikudanganye’, hajawahi kumshrikisha msanii yeyote katika nyimbo zake tangu alipotoka na ngoma yake ‘Nagusagusa’ kisha kufuatiwa na One Day.

No comments