Header Ads

Nawal Anatafuta Kiki Tena Ananitafuta Undani- Nuh Mziwanda

Nawal Anatafuta Kiki Tena Ananitafuta Undani- Nuh Mziwanda


KUFUATIA povu alilolitoa aliyewahi kuwa mke wa mwanamuziki Nuh Mziwanda, bidada Nawali kwenye kituo kimoja cha televisheni kwamba baba wa mtoto wake huyo hamuhudumii mtoto wao, Nuh amefunguka kuwa mwanamke huyo anatafuta kiki na si bure.

Akichonga na Uwazi Showbiz, Nuh alisema kuwa mara kwa mara amekuwa akiwasiliana na mwanamke huyo kumjulia hali mwanaye ikiwa ni pamoja na kumhudumia lakini anashangazwa na yeye kuibuka kwenye media na kudai hamhudumii.

“Mambo mengine unaweza kusema hata mtu anatafuta kiki au anakutafuta la undani. Kiukweli sitaki kulizungumzia suala hili sana lakini ukweli ni kwamba siwezi kuacha kumhudumia mwanangu! 

No comments