Header Ads

Manchester City yaviburuza vigogo vya Epl katika You Tube, United watia aibu


Inaonekana huu ni mwaka wa Manchester City ndani na nje ya uwanja, wakati klabu yao ikiwa inaongoza katika ligi kuu ya Epl sasa vinara hao wameweka rekodi nyingine nje ya uwanja katika mtandao wa You Tube.
Manchester City wanakuwa klabu ya kwanza kufikisha subscribers milioni 1 katika You Tube, hii ina maana chaneli ya You Tube ya Man City imefikisha watu milion 1.
Hii leo Man City walionesha live tukio hilo la kubwa klabu ya kwanza kufikisha idadi hiyo ya subsctibers huku kiungo wao Yaya Toure alikuwa live kuwashukurumashabiki wao kwa jambo hilo.
Lakini suala la kushangaza wakati Manchester City wakifikisha idadi hiyo ya subscribers, wapinzani wao wakubwa Manchester United wao hawana chaneli maalum katika mtandao wa You Tube.
Kiujumla Man City wana subscribers milioni moja na elfu nne huku Arsenal wakifuatia na subscribers laki saba na elfu kumi, nafasi ya tatu imekwenda kwa Liverpool wenye subscribers laki sita na tisini na nane.
Chelsea wanashika nafasi ya nne wakiwa na subscribers laki sita na tisini na tatu elfu huku Tottenham wakiwa na subscribers laki mbili na kumi na mbili elfu huku United wakiwa hawana chaneli You Tube.
Wakati Manchester City wakiviburuza vigogo wengine katika You Tube, msimamo wa Epl unaonesha Manchester City wanajinafasi kileleni mwa ligi wakiwa na alama 25 zikiwa ni alama 5 mbele ya United na Tottenham.

No comments