Mabao 7 ya Liverpool hii leo yavunja rekodi ya Manchester United na kuweka rekodi mpya, matokeo yote haya hapa
Hii leo ilikuwa mara ya kwanza kwa klabu ya Liverpool kufunga idadi ya mabao 5 katika mechi ya ugenini katika michuano ya Champions League, michezo yao 45 iliyopita ya Champioms League hawakuwahi kufanya hivyo.
Robert Firminho (4), Phellipe Coutinho (13) na Mohamed Salaah (19,40) waliufanya mchezo uende mapumziko huku Liverpool wakiongoza kwa mabao 4 kabla ya Firmninho kuweka la tano kipindi cha pili.
Na bao la 7 la Alexander Arnold likawafanya Liverpool kuwa timu ya nne kuwahi kufunga jumla ya mabao 7 na zaidi ambapo timu za Bayern Munich, Barcelona na Lyon zimewahi kufanya hivyo na isitoshe kwa usiku wa leo Liverpool ilikuwa timu pekee ambayo haikuruhusu bao.
Manchester City waliipiga Napoli bao 2 huku Gabriel Jesus akifunga moja ya bao linalomfanya kufunga mabao 15 ndani ya michezo 22 ikiwa ni mchezo mmoja nyuma ya Kun Aguero wakati anafunga mabao kama hayo alipofika Man City.
Bao la Papstathopoulos liliookoa Dortmund kutoka katika kipigo na kuwafanya kutoka sare ya moja kwa moja dhidi ya Apoel Nicosia, huku Monaco wakifungwa 2 kwa 1 na Bestikas katika uwanja wao wa nyumbani.
Post a Comment