Arsenal wampa mzee Wenger zawadi kubwa ya birthday kwa mara ya 3
Happy birthaday Arsene Wenger, leo ni siku ya kuzaliwa kwa kocha wa Arsenal Arsene Wenger na hii leo alikuwa akitimiza miaka 68, Wenger ametimiza miaka 68, rekodi zinaonesha Wenger ameahinda katika siku yake ya kuzaliwa mara tatu 2006,2014 na hii leo.
Alianza Wayne Rooney kufungua ukurasa wa mabao huku likiwa bao lake la 12 dhidi ya Arsenal katika Epl na la 15 katika michuano yote, idadi inayomfanya kuwa mchezaji ambaye amewafunga zaidi Arsenal katika Epl.
Alexis Sanchez aliwafungia Arsenal bao la tatu bao ambalo linamfanya kuwa mchezaji kutokea Ufaransa mwenye mabao mengi zaidi mwaka 2017 ambapo hadi sasa anakuwa amefunga mabao 27.
Aaron Ramsey alifunga bao la nne na Alexis Sanchez akafunga bao la tano na kuwafanya Arsenal kuwa timu ya kwanza kufunga mabao mengi zaidi dhidi ya timu moja baada ya leo kufikisha idadi ya mabao 100 dhidi ya Everton.
Post a Comment