Header Ads

Simba imetangaza kamati ya kumtafuta mwekezaji


Klabu ya Simba imetangaza kamati ya watu watano itakayosimamia mchakato wa kumpata mwekezaji katika mfumo mpya wa uendeshaji wa klabu hiyo.
Kamati hiyo inaundwa na Jaji mstaafu Thomas Mihayo, ambaye ameteuliwa kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo, wajumbe ni Mh. Mussa Azzan Zungu (MB), Abdulrazaq Badru, Dkt. Damas Ndumbaro na Yusuph Maggid Nassoro.
Ktika mfumo huo mpya asilimia 50 ya kampuni itakayoanzishwa, itatolewa kwa mwekezaji/wawekezaji atakaetokana miongoni mwa wanachama wa Simba kupitia mchakato wa zabuni.

No comments