Header Ads

Lulu Diva afichua siri ya weupe wake, ‘nakula sana mboga na matunda’





Msanii wa muziki Bongo, Lulu Diva amefichua siri ya weupe wake.
Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma yake ‘Give It To Me’ ameiambia Planet Bongo ya EA Radio kuwa weupe wake unatokana na kula mboga mboga na matunda.
“Msanii unatakiwa unaanza kuji-brand kuanzia mwili wako, ngozi yako, vitu unavyokula, naweza sema nakula sana mboga mboga na matunda na kuna baadhi ya vyakula vinasaidia ngozi kung’ara,” amesema Lulu Diva.
Katika hatua nyingine msanii huyo amezungumzia kolabo yake na ExQ kutoka nchini Zimbabwe na kueleza msanii huyo ndiye aliyemtafuta.
“Ndio kolabo yangu ya kwanza kushirikishwa tena kutoka nje, it’s means wameona Lulu ana uwezo anaweza kufanya kitu kikubwa that why wameweza kuniamini,” amesema.

No comments