Mtuhumiwa Samson Petro enzi za uhai wake.
MTUHUMIWA  Samson Petro anayedaiwa kuteka na kuua watoto wawili, Maureen na Ikram, amefariki dunia kwa kupigwa na risasi wakati akitaka kutoroka mikononi mwa Polisi jijini Arusha.
Mtuhumiwa alipigwa risasi mbili za miguu wakati akijaribu kutoroka na akafariki dunia akiwa Hospitali ya Mount Meru, Arusha.
Awali usiku wa tarehe 2 Septemba mwaka huu, mtuhumiwa mwenye umri wa miaka 18, alikamatwa na polisi kwa tuhuma za kuteka watoto katika mikoa wa Arusha na Geita.
(CHANZO: JAMIIFORUMS)