Header Ads

Roma Mkatoliki: Nikikutana na Rais Magufuli ntamuomba msaada huu


Rapa Roma Mkatoliki ameweka wazi akipata nafasi ya kukutana ana kwa ana na Rais John Pombe Magufuli, atakachofanya ni kumweleza tu shida zake binafsi ili asaidiwe kutimiza ndoto zake.

Roma Mkatoliki alisema hayo alipokuwa akiongea na EATV na kusema unapokutana na Rais kwa dakika chache ni fursa kubwa hivyo lazima uitumie vizuri kwani ukisema uanze kueleza matatizo ya wananchi unaweza kukosa nafasi ya kueleza mambo yako kutokana na kukosa muda.

No comments