Header Ads

Muuza ‘madawa ya kulevya’ atiwa nguvuni


Tokeo la picha la Luiz Carlos da Rocha 
Polisi nchini Brazil inamshikilia mlanguzi wa madawa ya kulevya maarufu Barani Amerika ya Kusini, Luiz Carlos da Rocha ambaye alifanyiwa upasuaji ili kukwepa kukamatwa kwa takribani miaka 30.
                                                                   Luiz Carlos da Rocha
Luiz Carlos da Rocha ambaye pia anafahamika kama “White Head” anaaminika kuongoza genge kubwa la madawa ya kulevya barani America Kusini.
Rocha alikamatwa eno la Sorriso katika jimo la magharibu la Mato Grosson siku ya Jumamosi.
Polisi walilinganisha picha zake za zamani za Rocha na za mshukiwa mpya na kusema kuwa Luiz Carlos da Rocha na Vitor Luiz ni mtu mmoja.
Kwa mujibu wa Sheria za nchi ya Brazil Rocha huenda akahukumiwa miaka 50 jela.

No comments