Mtibwa Sugar kuweka kambi Dar.
TIMU ya Mtibwa Sugar itapiga kambi ya wiki mbili jijini Dar es Salaam kujiandaa na msimu mpya wa Ligi Kuu Bara utakaoanza mwishoni mwa Agosti.
Afisa Habari wa Mtibwa Sugar, Thobias Kifaru akizungumza na alisema kambi hiyo itaanza Jumatano na wanaamini itawasaidia kufanya vizu ri kwenye msimu ujao wa ligi.
Kifaru alisema kwa asilimia kubwa wamemaliza usajili wao mabao wameufanya kwa umakini hasa kwa kusajili vijana ambao wanaamini wataipa mafanikio klabu hiyo.
“Tutaweka kambi ya mazoezi kwa wiki mbili Dar es Salaam mpaka Julai 28 na Julai 29 tutacheza mchezo wa kuwania kombe la Faith Baptist dhidi ya Mbeya City utakaofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri Morogoro na baada ya mchezo huo tutarejea Turiani kuendelea na kambi,”alisema Kifaru.
Msemaji huyo alisema baada ya wachezaji kadhaa kuondoka katika timu hiyo akiwemo beki Salim Mbonde na winga Ally Shomari waliotimkia Simba wamewaongeza wachezaji vijana kuziba nafasi zao wakiwemo Hassan Iddi kutoka Oljoro JKT na Salum Ramadhan kutoka Polisi Morogoro.
Post a Comment