Header Ads

COUTINHO NDIYE ATAKUWA MRITHI WA INIESTA ATAKAPOTUA FC BARCELONA


Imeelezwa mpango wa Barcelona kutaka kumsajili Coutinho wa Liverpool ni kumrithi Andres Iniesta.


Barcelona wanaamini mkongwe huyo anahitaji msaada, ndiyo maana wameendelea kuwekeza nguvu zao kwa Coutinho.

Pamoja na mambo kuwa kimya lakini Barcelona inaonekana imepania hasa kumaliza kila kitu na kumpata Coutinho.

Kuna mikutano mfululizo imekuwa ikiendelea kuhusiana na Coutinho kujiunga na Barcelona na hivi karibuni, kampuni ya Nike inayoitengenezea Barcelona jezi, ilivujisha jezi ya Coutinho jambo ambalo limetoa picha mambo yanaweza kuwa mazuri kwa klabu hiyo maarufu duniani.

No comments