Header Ads

Nou Camp kubadilishwa jina kuanzia msimu unao.


Klabu ya Barcelona inataraji kubadili jina la uwanja wao wa sasa wa Nou Camp na kuwa “Nou Camp Grifol” jina ambalo litaanza kutumika katika msimu ujao wa ligi wa 2018/2018.
Barcelona wamekubali kubadili jina hilo baada ya kusaini dili na kampuni inayohusiana na masuala ya madawa na kemikali iitwayo Grifol ambapo dili hilo linatajwa kuwa na thamani ya zaidi ya kiasi cha £340m.
Makataba wa Grifol na Barcelona utawafanya Grifol kulipia marekebisho ya uwanja wa sasa wa Barcelona lakini vile vile mkataba huo wa Grifol unaweza kutumika katika mkataba mpya wa Lioneil Messi.
Redio mmoja nchini Hispania usiku wa jana ilitangaza dili hilo na kusema Grifol wako tayari kutoa kiasi £535m kwa ajili ya matanuzi na kuuboresha upya uwanja wa sasa wa Barcelona.
Dili hili linataraji kuwaboost Barcelona katika mkataba mpya wa Lioneil Messi ambaye hadi sasa hajasaini mkataba mpya kutokana na kiasi kikubwa cha pesa ambacho Messi anataka kupewa katika mkataba huo.

No comments