MWANAMITINDO maarufu Bongo, Jokate Mwegelo amesema kuwa, atahakikisha anapambana vilivyo kwa ajili ya kutetea haki ya mwanamke pamoja na watoto kwa ujumla.

Akizungumza na Star Mix, Jokate alisema, kuna umuhimu sana kila mmoja mwenye nafasi kwenye jamii atambue nafasi ya mwanamke kwani wao ndio wenye nafasi kubwa kwenye jamii na pia kukazania kuwapa elimu.

“Unajua watu wengi wanajisahau kuhusu mwanamke na watoto lakini kwa upande wangu naona thamani kubwa sana ya mwanamke hasa akipatiwa elimu bora na kupewa nafasi nyingi za kuongoza huku watoto wakipewa haki inayostahili,” alisema Jokate.