Header Ads

Hemedy PhD akana kufuata ‘totozi’ Bongo Movie





Msanii wa muziki Bongo na muigizaji wa Filamu, Hemed PhD amesema si kweli aliingia Bongo Movie kwa ajili ya kufuata warembo.
Muimbaji huyo ambaye kwa sasa anafanya vizuri na ngoma ‘Mkimbie’ ameiambia The Playlist ya Times Fm kuwa aliingia Bongo Movie baada ya kufanya vizuri Tusker Project Fame ndipo baadhi ya madirector wakamshauri kuingia katika movie.
“Hapana, ilikuja baada ya kuachia single yangu ya kwanza “Ninachotaka’ jamaa walikua wanaona vile ninavyofanya toka project Fame, nipo kwenye house kwa sababu ile show ilikuwa inaenda kama Bing Brother fulani,” amesema Hemedy.
“Kwamba kuna maisha kwenye nyumba halafu kuna performance yale ya maisha ya kwenye nyumba zile drama ziliwavutia wale madirector wakanitafuta, hao watoto walikuja to a long the way,” ameongeza” ameongeza.

No comments