Header Ads

TAIFA STARS YAITWANGA BOSTSWANA 2-0, MSUVA APIGA ZOTE AKIONYESHA UTAMU WAKE WA MOROCCO





Taifa Stars imeshinda kwa mabao 2-0 katika mechi yake ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Botswana.

Katika mechi hiyo kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, Simon Msuva ndiye aliyefunga mabao yote mawili.

Msuva aliyepata umaarufu akiwa Yanga, sasa anakipuga Difaa Al Jadid ya Morocco na alichelewa kujiunga na wenzake.

Lakini leo alionyesha kuwa uhai wa timu katika ushambulizi huku akipiga mabao hayo mawili safi kabisa.

No comments