Header Ads

STAND UNITEDA WASEMA WATAIFUNGA SIMBA WAIPE SOMO LA USAJILI WA WAZALENDO



Stand United wametamba wataifunga Simba ili kuwaonyesha thamani ya wachezaji wa Kitanzania.

Mwenyekiti wa Stand United, Elson Maeja amesema wako tayari na wamepania kuwatwanga Simba ili kuwaonyesha wachezaji wa Simba.

Stand United imetoka nje ya mji wa Shinyanga na kwenda Wilayani Kahama katika eneo la Irogi kuweka kambi wakisubiri mechi yao ya Ligi Kuu Bara, Jumamosi.

“Hawa Simba wamekuwa wakisajili wachezaji wa kigeni kwa gharama kubwa. Utendaji wao hauna tofauti na wachezaji wa Kitanzania.

“Sasa tunataka kuwafunga ili waheshimu Wazalendo na waachane na kusajili wachezaji wa majimaji tu,” alisema.


Stand United wamesisitiza wanataka kuchukua pointi hizo tatu kutoka Simba ili wajiweke vizuri.

No comments