Header Ads

Shilole Hausiki Kuvunja Ndoa Yangu Bali ni Wazazi wa Nawal- Nuhu Mziwanda

Shilole Hausiki Kuvunja Ndoa Yangu Bali ni Wazazi wa Nawal- Nuhu Mziwanda


Mwanamuziki Nuh Mziwanda amekanusha suala linaloongelewa na watu kuwa kuvunjika kwa mapenzi kati yake na mzazi mwenzie chanzo chake siyo Shilole bali ni wazazi wa binti huyo.

“Unajua watanzania ukiwapa picha tu, basi wao wataandika maneno wataandika wenyewe Shilole hausiki hata kidogo kuvunjika kwa mahusiano yangu.”

“Wahusika ni wazazi wake ambae yeye aliamua kuwasikiliza wazazi wake kwa kuolewa na mtu mwingine na hatukuwa na ugomvi wowote ila ndio hivyo wazazi walikuwa na nguvu sana kunizidi mimi,” aliongeza.

Aidha Nuh Mziwanda aliongeza kuwa mahusiano yake ameyaweka kando na yupo kupambana na hali yake, lakini anashukuru Mungu mtoto wake bado anaendelea vizuri na anapata taarifa zote muhimu kumuhusu mtoto wake lakini mengine imebaki stori. 

No comments