Header Ads

QUICK RACKA: MIMI NA KAJALA ZILIPENDWA TU!


Quick Racka na Kajala.
MSANII wa Bongo Fleva, Aboot Racka ‘Quick Racka’ amefunguka kuwa yeye na staa wa filamu Bongo, Kajala Masanjawamebaki zilipendwa tu na kila mmoja anaangalia ustarabu wake mwingine.
Akizungumza na Ijumaa, Quick aliyekuwa gumzo baada ya kutoka na Kajala alisema, katika maisha yake amepanga kamwe hawezi kuoa mwanamke staa au ambaye yuko nae kwenye tasnia moja ya muziki.
“Mimi na Kajala tumebaki zilipendwa tu na wala sina mpango wa kumuoa kama ulivyosikia zamani bali kama nitakuja kuoa basi nitaoa mwanamke ambaye hajulikani kabisa kwenye jamii yetu inayotu-zunguka,” alisema Quick.

No comments