Header Ads

Picha: Dillish wa BBA aliyedaiwa kutoka na Diamond adai ana mimba


Mshindi wa Big Brother Afrika mwaka 2013 kutoka Namibia, Dillish Mathews inasemekana kuwa ni mjamzito.
Mrembo huyo ambaye hivi aliingia kwenye tetezi za kutoka kimapenzi na Diamond, ameibua mapya baada ya kuweka picha katika mtandao wa Instagram akiwa kashikilia tumbo huku akiuliza kuwa ni mtoto au baga?

Hali hiyo imeibua mengi na watu wengi wamehisi kwamba kama Dillish ni mjamzito basi itakuwa Diamond Platnumz anahusika kwa sababu inasemekana kuwa alikuwa na uhusiano na mrembo huyo hivi karibuni.
Kama ni kweli basi hali inaweza kuwa tata, kwani tayari kuwa baadhi ya watanzania wapo katika page ya mrembo huyo wakishaa taarifa hiyo.
Diamond ambaye ni baba wa watoto wawili kwa Zari, hivi karibuni amepata mtoto wa tatu kupitia mwanamitindo, Hamisa Mobetto.

No comments