Header Ads

PENDO AIBUKA, ATAJA SABABU ZA KUCHUKIA MAPENZI!


Upendo Mushi ‘Pendo’.
MSANII wa filamu ambaye ni zao la Shindano la Maisha Plus Season 1, Upendo Mushi ‘Pendo’, amesema kuwa, sababu zinazomfanya aishi bila mwanaume ni kutokana na kuumizwa na wanaume ikiwemo ndoa yake ambayo aliolewa na kuachika kimyakimya mwishoni mwa mwaka jana.

Katika kubadilishana mawazo na mwandishi wetu kuhusu maisha, Pendo ambaye aliwahi kung’ara na marehemu Kanumba kupitia Filamu ya Moses, aliweka wazi namna ambavyo alikutana na mateso makali kwenye ndoa yake na kwamba kwa sasa anaona kuishi peke yake ni bora kuliko kuingia kwenye uhusiano ambako kuna maumivu na vilio visivyokauka.

“Unaona ninavyoishi hivi mwenyewe, nafurahia maisha maana nimeumizwa mpaka basi, niliingia kwenye ndoa kimyakimya, lakini haikudumu tukaachana, kwa sasa niko huru kabisa,” alisema Pendo.
STORI: BRIGHTON MASALU | GAZETI LA AMANI

No comments