Header Ads

Oxlade Chamberlain kwenda Liverpool ni usajili wa kisoka zaidi kuliko pesa


Neymar amekwenda PSG kwa rekodi ya dunia ya £220m, Osmane Dembele akaenda Barcelona waweka mzigo wa £160m,Morata Chelsea wakatoa £70m na United nao wakatoa £90 kumnunua Lukaku.
Hilo ndio soka mwanangu, pesa mbele mapenzi baadaye. Wachezaji wote hao hapo juu na wengine wengi wamevutiwa sana na kiasi cha pesa ambacho wameahidiwa japo ukubwa na historia za klabu walizoenda pia ni sababu.
Mpira wa sasa upo kibiashara zaidi na mwenye biashara nzuri ndio atafaidika, soka la sasa limekuwa na vijana ambao wanaangalia zaidi maslahi na ndio maana haikushangaza ligi kuu nchini China ilipoanza kuwatishia vigogo wa Ulaya, ndioo lazima wawatishe kwa sababu wana pesa.
Nchini Uingereza inaonekana vijana wengi wadogo waliokulia Southampton wanapaona Anfield kama sehemu nzuri zaidi kutamani kwenda na ndio maana haikuwa ngumu kwa Ricky Lambert, Adam Lallana, Nathan Clyne na hata Sadio Mane kukubali kujiunga na Liverpool.
Shabiki mmoja alifanya mzaha na kusema Liverpool walitaka kutoa £35 kumnunua Chamberlain wakati hawajui alipitia Southamoton lakini walipojua tu aliichezea Southampton hapo hapo wakazama mfukoni wakatoa £40m.
Ni utani lakini kama kweli kwani pamoja na wachezaji wanaotokea Southampton kuvutiwa na Liverpool lakini inaaminika Liverpool wanawaona vijana wa Southampton kama watu sahihi na wanaoweza kuibeba Liverpool moyoni na kupambana kwa ajili ya klabu.
Unadhani Chamberlain hajui kwamba Chelsea wangempa mshahara wa zaidi ya £180,000? Au unadhani Chamberlain hafahamu kwamba Arsenal wangempa £185,000? Anajua sana kwamba angepiga pesa nyingi lakini kwanini akatae pesa zote hizo na akubali £120,000 ndani ya Liverpool?
Jibu ni rahisi sana kwa mzaliwa huyu wa Portmouth, hakutaka pesa! Ox alitaka akaipiganie klabu ambayo aliamini tangu akiwa kijana mdogo kwamba ndio klabu sahihi kwake, Chamberlain anaipenda Liverpool na hakutaka pesa za Chelsea huku akiwa kachoshwa na mzee Wenger.
Baada ya michezo 198 na mabao 20 sasa Ox anatarajiwa kwenda kujenga safu ya ushambuliaji yenye kasi mno pale Anfield huku akicheza na viberenge wengine Mohamed Salah na Sadio Mane, huyo ndio Chamberlain na £40m zinampeleka Anfield kucheza soka na sio kufanga biashara.

No comments