Siku chache zilizopita mmoja kati ya wanamitindo wanao kiki zaidi kibongo bongo Gigy Money alikichafua katika mitandao ya kijamii baada ya kutupia picha katika page yake ya Instagram ikimuonyesha akiwa na Diamond Platnumz katika pozi flani la kimitego mitego.
Kilichozua gumzo zaidi katika posts hizo ni caption za Gigy Money zilizo onyesha dhahiri kuwa mrembo huyo anamzimikia mtu mzima Diamond.
Sasa leo kwenye XXL ya Clouds fm Soudy Brown aliamua kumvutia waya Gigy Money kwenye U-Heard na kuamua kumuuliza juu ya utata huo ambao anauzua mitandaoni kuhusu yeye na Diamond Platnumz.
Gigy Money amethibitisha ni kweli yuko serious anamtamani Diamond kutoka naye kimapenzi na wala hajali kama yeye ana familia au vipi.
Katika maongezi ya Soudy Brown na Gigy MoneyGigy ameweza kufunguka kuwa tayari Diamond Platnumz amekwisha onyesha utayari wa kutoka naye kimapenzi ila mambo mengine yanatakiwa kubaki kuwa siri.