Header Ads

Tupa kule akina Pogba na Mbape, tazama majembe yaliyostaili zaidi ya €95 ila bahati mbaya yamestaafu


Dunia ya soka imeelekeza macho kwenye usajili huku Magazeti na Blog mbalimbali ikitawaliwa na tetesi za usajili pamoja na taarifa kamili za nani kaenda wapi na nani kavutwa wapi. Cha kushangaza ni kwamba kuna baadhi ya Wachezaji wanathaminishwa kwa pesa kubwa tofauti na uwezo na mafanikio yao pia. Leo hii vijana kama akina Mbape wanatajwa
kuwa na thamani ya paundi zaidi ya 100 jambo ambalo nitakuwa wa mwisho kulikubali.
Binafsi nilibahatika kutazama viwango vya baadhi ya wachezaji ambao walikuwa na uwezo mkubwa ila thamani kipesa ilikuwa ya kawaida labda kwa sababu ya nyakati pia.
Thiery Henry ni moja kati ya washambuliaji wachache ambao Dunia inawamisi kwa kipindi hiki ambacho akina Mbape ndio wanaonekana watu hatari katika eneo hili. Mzee Wenger huenda anajuta kumjua Henry kipindi kile kwani huu ndio ulikuwa wakati sahihi wa Henry kuwepo Arsenal kwa maana kubwa mbili, moja ni kwamba Arsenal haijapata mshambuliaji wa kueleweka tangu aondoke ‘Mheshimiwa’ Robin Van Persie na hii imefanya heshima ya Arsenal kupotea kabisa, pili kwa jinsi ‘Professor’ Wenger alivyo mchumi angeweza kutengeneza pesa chafu kwa kumuuza ‘Chogo boy’ kwingineko.
Henry aliyeichezea Arsenal mechi 254 kuanzia mwaka 1999 hadi 2007 aliweza kufunga magoli 174 huku dunia ikinyoosha mikono juu ishara ya kumpa heshima kama miongoni mwa ‘icon’ wachache wa Arsenal. Naamini uwezo wa Henry kwenye eneo la hatari la timu pinzani ulistahili mchezaji huyu kuuzwa zaidi ya paundi milioni 90 kama zama zile zingekuwa sasa. Ila cha ajabu ni kwamba Henry aliuzwa Barcelona kwa €24 million.
Ronaldinho ni zaidi ya mchawi wa mpira aliyepata kuonekana katika zama zake. Wakati nyie mkiwa bize kubishana ni nani bora kati ya Messi na CR7 mi nacheka kwa dharau maana nilibahatika kumfaidi Mchawi huyu aliyekuwa anatukosha kwa tabasamu lake muda wote wa mchezo. Gaucho alipiga chenga zote ambazo Messi kazipiga, Gaucho alifunga magoli yote
ambayo CR7 kafunga. Heshima anayopewa sasa pale Barcelona ni ndogo sana kulingana na shughuli nzito aliyoifanya kipindi yupo katika ubora wake.
Naamini hata Okocha alikuwa anajaribu kuyafanya yale ambayo Gaucho amesha yafanya.
Unadhani ingelikuwa zama hizi bei halisi ya Gaucho ingekuwakiasi gani? Wallah naapa bei ya chini kabisa ingekuwa £200 millioni anaebisha aje kwa hoja yenye mashiko na sio ya kishabiki. Thamani pekee ya goli la free-kick kutoka yadi 40 alilowafunga England chini ya mlinda mlango David Seaman ni takribani paundi 20 millioni. Gaucho alicheza Barca kuanzia 2003 hadi 2008 huku katika michezo 145 akifunga magoli 70 ila kumbuka huyu alikuwa kiungo mshambuliaji. Baada ya kuipiga chini ofa kutoka Man City, Gaucho alisaini Milani kwa  €22.05 millioni.
Raúl González Blanco. Teh teh teh teh najikuta nacheka nikisikia Mbape ana thamani ya paundi 100 millioni. Hivi ni nani aliyekuwa anamjua mshambuliaji huyu ambaye ilifika kipindi wahispania walitaka wamaubudu?  Raul alishinda mataji mengi sana na aliweza kudumu kwenye kikosi cha Madrid licha ya kuwepo kwa washambuIiaji hatari kama Ronaldo de Lima. Kiwango cha mshambuliaji huyu hakikuwahi kufikiwa na mshambuliaji yoyote wa Hispania japo Tores alijaribu kwa kadiri alivyoweza katika ngazi za vilabu na timu ya taifa. Raul nyavu zilikuwa zinamuogopa kwani hakuwa na masikhara langoni.
Raul angekuwa zama hizi zenye utani na pesa naamini bei yake ingekuwa zaidi ya paund 95 million na hili halina shaka hata kidogo. Kiwango chake kilimfanya atajwe na FFHS  kama mshambuliaji bora mwaka 1999, huku pia akitajwa kama mshambuliaji bora wa UEFA mara tatu mfululizo 2000, 2001 na 2002. Unadhani heshima hii ni mshambuliaji gani wa zama hizi kapewa? Leo hii kijana mdogo ambaye ana uwezo wa kawaida anauzwa paundi 100 millioni.
Ronaldo de Lima alimaliza karia yake kwa kufunga magoli 352 katika michezo 518. Ni mtu anayestahili heshima na lau kama anaona vijana kama akina Mbape wanatajwa kuwa na bei ya paund zaidi ya 100 atakuwa anashika mdomo kwa mshangao mkubwa huku akitamani zama za nyuma zirejee sasa na yeye aonekane kijana mbichi aliyemtungua Oliver Khani pale Japan mwaka 2002. Mikasi aliyokuwa anapiga CR7 inawezekana Ronaldo alikuwa anaitazama kwenye luninga huku akicheka kwa kejeli kwani hakukuwa na jipya kwa CR7. Ronaldo alikuwa na uwezo ambao hadi kesho Brazili itajivunia jina lake.
Licha ya nyota yake kuonekana mapema, Ronaldo hakulewa sifa, alikuwa na uwezo wa ‘ku-driblle’ uwezo wa kupiga chenga, kasi na mmaliziaji mzuri. Niambie ni mshambuliaji gani wa sasa mwenye sifa hizi.
Inawezekana Messi na CR7 wakajaribu ila bado wamekopi vitu vingi kutoka kwa Jembe hili ambalo liliichezea Brazil mechi 98 na kufunga magoli 62. Real Madrid ilimnunua kwa kiasi cha €46 milioni kutoka Inter huku mauzo ya jezi yake yakivunja rekodi. Nadhani angekuwepo leo thamani yake ingekuwa zaidi ya  €150.
Kwa leo namalizia na fundi mwingine ambaye anayo heshima yake pale Ufaransa. Zinedine Zidane hawezi kusahaulika milele pale Ufaransa na Madrid. Zidane alikuwa na uwezo mkubwa mno na angekuwepo leo hii naamini mshahara anaopokea CR7 ungekuwa halali yake. Zidane angekuwa na thamani kubwa zaidi ya Pogba. Goli alilowafunga Levekusen kwenye fainali ya UEFA bado vijana wa sasa wana deni la kulipa licha ya kupewa thamani kubwa wasiostahili. Kiungo huyu mchezeshaji alikuwa na chenga za dharau na uwezo mkubwa wa kushambulia timu pinzani.
Japo hakufunga sana katika vilabu alivyocheza ila alifanya makubwa ambayo daima tutaiheshimu thamani yake. Zidane hatojilaumu sana kwani €77.5 million alizonunuliwa akiwa Juve kwenda Madrid hazikuwa haba ila naamini angelikuwepo leo tungekuwa tunazungmza mengine. Uwezo wake akiwa kocha hautofautiani sana na alivyokuwa uwanjani.

No comments