Header Ads

Baada ya Draw, hii ni ratiba rasmi ya 16 bora Ndondo Cup 2017


Usiku wa Julai 10, 2017 ilichezeshwa draw ya Sports Extra Ndondo Cup 2017 kupata timu zitakazo kutana kwenye hatua hiyo baada ya timu 16 kufuzu hatua hiyo kutoka kwenye makundi.
Zoezi la kuchezesha draw lilifanyika live kupitia Sports Bar ndani ya Clouds TV na lilikuwa live pia kupitia youtube kwenye Dauda TV hivyo watu wengi walipata fursa ya kutazama.
Kwanza nikupe fursa ya kuzifaham timu 16 ambazo zimefanikiwa kuingia hatua ya mtoano (16 bora Ndondo Cup 2017). Ukiangalia hapa chini utapata kuzifahamu timu zote ambazo zimetinga hatua hiyo.
Baada ya zoezi la draw kuchezeshwa, kila timu sasa inajua itacheza na nani kwenye hatua ya 16 bora kwa maana nyingine ni kwamba kila mtu anamjua mpinzani wake kilichobaki ni kujiandaa kujua namna ya kumkabili.
Mechi za 16 bora zitaanza kupigwa Julai 16 2017 huku mechi ya ufunguzi kwenye hatua hiyo ikiwa ni kati ya Buguruni FC vs Goms United mechi ikipigwa kwenye uwanja wa Kinesi.

No comments