Header Ads

Ajali ya ndege yauwa watu 16




Watu 16 wamefariki papo hapo kwenye ajali ya ndege ya jeshi huko Mississipi nchini Marekani.
A still image showing a crashed plane in flames in a field, taken from video footage
Mabaki ya Ndege yakiteketea kwa moto
Ajali hiyo ilitokea katika Kaunti ya LeFlore karibia kilomita 160 kusini mwa mji mkuu wa jimbo hilo, Jackson.
Kwa mujibu wa mtandao wa Shirika la utangazaji la Reuters Watu wote 16 waliokuwa ndani ya ndege hiyo waliangamia huku chanzo cha ajali kikiwa  bado hakijafahamika.
Hata hivyo jarida la kiserikali la  jimbo la Mississipi limeandika kuwa ndege hiyo ilianguka katika shamba moja na mabaki yake kutapakaa maeneo tofauti tofauti.
Ndege hiyo yenye namba KC-130 ni moja ya ndege za kijeshi zenye gharama kubwa zinazotumiwa na Jeshi la majini la Marekani kwenye nyakati tofauti.
Tokeo la picha la kc-130 marines
Mfano wa ndege iliyopata ajali KC-13J Marines

Kupitia ukurasa rasmi wa twitter wa Jeshi la Majini wamethibitisha taarifa hizo huku wakieleza kuwa taarifa zaidi zitatolewa kesho kuhusu ajali hiyo.

No comments